#2.
Maswali matatu ya msingi.

JE! NI VIZURI KUMHOJI MTU HUYU, KWA WAKATI HUU NA MAHALI HAPA?

Kutathmini usalama wa wanaohojiwa ni jukumu la wanahabari katika ngazi zote ikimo mwandishi aliye uwanjani, mhariri katika chumba cha habari na wenzake wanaofuatilia habari hiyo hiyo.

Wakati wa kuripoti kuhusu ukatili wa kijinsia kwenye migogoro, wanahabari wanahitaji kufanya tathmini ya hatari juu ya usalama wa wale wanahojiwa, kama vile wanavyofanya tathmini ya usalama wao wenyewe. Maswali ya msingi juu ya uangalifu unaofaa ni pamoja na: 

  • Je, ninao muda wa kutosha kufanya mahojiano haya vizuri? Mazungumzo ya aina hii hayapaswi kuharakishwa. Ikiwa sivyo, nitawezaje kufanya mambo tofauti ili kuepuka kusababisha madhara yoyote?
  • Je, mazingira haya ni salama? Nani amehudhuria kwenye chumba na ni nani hapaswi kuhudhuria? Je, ninaelewa mienendo ya nguvu za kisiasa kikamilifu ili kuweza kutathmini athari zinazoweza kutokea kwa wale ninaowahoji? Je, kuna aina yoyote ya kulazimishwa?
  • Je, mtu huyu ndiye mtu anayefaa kuhojiwa? Je, mhasiriwa yuko tayari kihemko kufanya mazungumzo haya? Na ikiwa sio, ni nani anayeweza kuwa tayari?

Huenda umesafiri njia ndefu kwa hatari kubwa ya kibinafsi, lakini wakati mwingine maadili ya hali yanaweza kuhitaji mpango mpya. Wahariri pamoja na waandishi walio nyanjani wanahitaji kuchukuwa jukumu la hii – Je! mazungumzo haya ya tasaidiya?

Je, ninao muda wa kutosha kufanya hii kazi? 

Wanahabari hufanya kazi chini ya shinikizo kubwa la wakati. Lakini kumhoji mhasiriwa wa ukatili wa kingono unahitaji wakati wa kutosha. 

  • Lazima uwe na muda wa kukaa wa kutosha wa kumhoji aliyenusurika. 
  • Ikiwa huna wakati wa kutosha, unaweza kupanga tena siku yako? 
  • Je, unaweza kufanya mahojiano hayo kwa njia tofauti kwa mfano, kwa kuuliza maswali ya uhakika badala ya kumfanya mhasiriwa kuelezea fedheha aliyoipitia?
  • Au unapaswa kumhoji mtu anayehusika lakini ambaye hakushambuliwa kwa nia ya moja kwa moja?

Aina hii ya mipango inaweza kuhusisha watu wengine wasiokuwa wewe mhasiriwa. Ikiwa mahojiano hayo yanapangwa kupitia mpatanishi kama vile asasi isiyo ya serikali au kikundi cha wazee wa eneo, waeleze kuhusu muda utakao kuwa nao ili uweze kupanga mambo yako ipasavyo.

Unaweza pia kumshirikisha mhasiriwa katika upangaji, kadri inavyowezekana. Ikiwa ratiba yako ni rahisi kubadilika, muulize mhasiriwa kwa mapema ikiwa kuna wakati mzuri wa kuongea, wakati ana nguvu zaidi kwa sababu yanaweza kuwa mazungumzo ya kuchosha. Kumpa mtu unayemhoji nafasi ya kubadili mpango ni njia rahisi lakini yenye nguvu ya kumfanya ajisikie kama ana udhibiti wa habari anayoitoa.

Je, mahali hapa ni salama kwa mahojiano? 

Labda umezoea kufikiria juu ya usalama wa maeneo ambayo unafanyia kazi. Lakini linapokuja suala la kumhoji nusura, unapaswa kufikiria zaidi ya haya. Anza kwa kujiuliza maswali rahisi kama vile nani  atakuwepo ndani ya chumba na kwa nini:

  • Je, kuna watu wenye bunduki?
  • Je, kuna wazee wa jamii?
  • Je, kuna watu ambao wanahusiana na mitandao ya wahalifu?
  • Je! Kuna mtu yeyote ambaye haitaji tu kuwa hapo?

Hata kama wahusika wa vurugu hawahudhurii kwenye chumba; jiswali piya kama wanaishi katika jamii, Je! habari kuhusu mahojiano hayo inaweza kuwafikiya?

Usirudishe wahasiriwa mahali kitendo kilitokea isipokuwa uwe unajua unachofanya. Hali hii inaweza kusababisha athari kali za kiwewe. 

Ingawa inaweza kuwa vigumu kupitia hali ya aina hii, kumbuka kuwa wewe ndiye unadhibiti mahojiano, na ikiwa inaonekana imeshurutishwa, au kuna uwezekano wa kumueka mhasiriwa hatarini, unapaswa kusimamisha mahojiano hayo. Wahariri wana majukumu yao pia kwa sababu shinikizo kutoka kwa chumba cha habari linaweza kuathiri akili ya mwanabari anapokabiliwa na changamoto ya maadili.

Huenda pia kuna wasaidizi ambao umekuja nao:

  • Ikiwa wewe ni mtangazaji, je, unaeza kuja na wasaidizi wachache iwezekanavyo?
  • Ikiwa unafanya kazi na mpiga picha, je, anaweza kuchukua picha baada ya mahojiano ili yule mhasiriwa asipigwe picha wakati anazungumzia matukio?
  • Ikiwa unafanya kazi na mkalimani, je, ni mtu anayestakihi kwa kazi hiyo? Je, mkalimani anaelewa masuala hayo na je, amepewa maelezo kuhusu mahojiano ya aina hiyo?
  • Je,  mhasiriwa anajisikia nafuu kuzungumza na watu wa jinsia tofauti kwenye chumba cha mahojiano? Sio lazima kwamba wanawake wawahoji wanawake, au wanaume wawahoji wanaume, lakini hii ni jambo la kuzingatia.
  • Hata kamaa anayehoji ni mwanamume wenye hisia nzuri, katika hali nyingi, mhasiriwa wa kike anaweza kujisikia salama akihojiwa na mwanamke mwenzake; ikiwa hiyo haiwezekani, inafaa kuwa na mwenzako wa kazi wa kike  karibu. (Kuhoji watoto na vijana kuhusuunyanyasaji wa kijinsia kunahitaji utaalamu na bidi ya ziada. Kila mara jiulize ikiwa hii kweli ni jambo ambalo unapaswa kufanya).
  • Ikiwezekana, muulize mhasiriwa ni nini anapendelea. Je! kuna mtu yeyote ambaye mhasiriwa anataka awe naye hapo, kama jamaa au rafiki wa kuaminika? Ikiwa unamhoji mtoto mdogo, mlezi wake anapaswa  kuwepo.

Je, huyu mtu anafaa kuhojiwa?

Ambayo inayoweza kuwa Jiulize maswali haya rahisi:

  • Je!  mhasiriwa huyu yuko thabiti na katika hali inayofaa kuzungumza?
  • Je! yuko katika hali inayofaa kuzungumza? Ni nini matarajio yake na je, ni matarajioyao ni yapi. Yanayowezekana?
  • Je! unahitaji mahojiano haya? Je! yanaongeza chochote au unayo habari ya kutosha?

Mara nyingi, katika mazingira ya migogoro au ya baada ya vita, asasi zisizokuwa za serikali zinazofanya kazi nyanjani ndizo zinapatanisha wanahabari na huenda  ndio wamekupangia kuzungumza na wahasiriwa wa ukatili wa kingono. Unaweza kujikuta kwamba asasi isiyokuwa ya serikali inaanda mtu yule yule au kikundi kidogo cha watu kwa ratiba finyo ya mahojiano na wanahabari. Kurudia hadithi tena na tena kwa muda mfupi inaweza kuwa ya kuchosha sana kwa mtu ambaye amepata kiwewe. Inaweza pia kuwa na athari za kisheria kwa mhasiriwa Ikiwa katika mahojiano tofauti mhasiriwa ameongea mambo yanakinzana kidogo, hili linaweza kudhoofisha nafasi zao za kutafuta suluhisho la kisheria baadaye.. [see box / ref to location].

Kwa kuzingatia shinikizo la wakati ambalo wanahabari wanakumbwa nalo, ni rahisi kukubaliana na yale ambayo asasi zisizokuwa za serikali zitapendekeza. Lakini inafaa kuwa na mazungumzo kuhusu matakwa wanayowekewa wahasiriwa wakati unaowahoji. Unaweza kuwauliza ni mara ngapi wamehojiwa. Kuwa mbunifu – ikiwa unasafiri katika kundi la wanahabari, mnaweza kushirikiana katika utafiti wenu ili yule mhasiriwa aweze kuhadithia habari yake mara moja tu.

Akizungumza na Columbia Journalism Review mnamo mwaka 2019, Skye Wheeler wa shirika la Human Rights Watch alielezea juu ya vitendo visivyo vya maadili vya uanahabari na vya utafiti vilivyo fanyika kwa wahasiriwa wa ukatili wa kijinsia katika kambi za wakimbizi za Rohingya nchini Bangladesh: 

“Bila shaka tunaweza kuangalia nyuma na kusema mambo hayakwenda sawa. Watu walihojiwa mara nyingi,” alisema Sky. [a]

Zingatio la muhimu-ambayo inaweza kuwa ngumu kuhukumu ni kama mtu tayari anajisikia salama kisaikolojia kufanya mahojiano. Bado wanaweza kuwa wanahisi mfadhaiko ikiwa tukio hilo la kutisha lilitokea hivi karibuni. Kuna uwezekano mkubwa pia kuwa ukatili wa kijinsia haukutendeka bila matukio mengine – mhasiriwa anaweza kuwa amepitia aina nyingine za vurugu, amepoteza watu wa familia, au kuhamishwa kwa lazima. Kwa ufupi, je, wako katika hali ambayo wanaweza kuzungumza?

Inaweza kuwa shida kubwa kutathmini usalama wakihemko na wa kimwili kwa unayemhoji na pia kwako mwenyewe. Suluhisho mara nyingi ni kuwahusisha watu kikamilifu katika kupanga vile mahojiano yatakuwa, na kuwapa udhibiti juu ya jinsi yatakavyofanyika. Masuala haya mengi yanaingiliana na swali la idhini. Maelezo zaidi juu ya hilo tutayapata katika sehemu inayofuata.

Unyanyapaa na jinsi kuripoti inaweza kuharibika

Jiulize ikiwa kumhoji mtu flani kunahatarisha usalama wake na faragha. Katika jamii zingine, mtu akishukiwa kubakwa, inaweza kusababisha udhalilishaji, kutengwa na hata kusababisha vurugu zaidi. 

Hapa kuna mfano kutoka Iraq kuonyesha jinsi mambo yanaweza kuharibika wakati wanahabari hawajafahamishwa kikamilifu kuhusu hali halisi. 

Johanna Foster na Sherizaan Minwalla walichunguza mahojiano 26 ya maoni ya wanawake wa Yazidi juu ya hali na athari za kuripoti kuhusu wanawake na wasichana ambao walinusurika utekwaji, ubakaji, na usafirishaji haramu wa ISIS. Waliweka matokeo yao katika utafiti mwaka 2018. Hapa kuna dondoo muhimu:

“Kama wanawake wengi ulimwenguni, wanawake wa Yazidi wanakabiliwa na shida ya kawaida ya kijinsia ya kuulizwa kutanguliza mahitaji ya jamii kuliko yao wenyewe. 

“Hasa, walikuwa wanakabiliwa na uamuzi wa kujitolea kuhadithia matukio yao ya kufedhehesha kwa ulimwengu, licha ya hatari za kibinafsi, za mwili, sifa, na kihemko. Kwa kweli, wanawake wa Yazidi walihimizwa moja kwa moja kufanya hivyo na wanaume wa wa jamii yao bila hakikisho kwamba hawatanyiwa unyanyapaa kwa kupoteza heshima yao au kutendewa vibaya au kukataliwa na familia zao na jamii, haswa baada ya muda kupita.”

Mmoja wa wanawake wa Yazidi aliyehojiwa alisema:

“Mwanzoni, niliporudi [kutoka ISIS], kamati ilikuja na kinasa sauti na kusema tutarekodi kisa chako. Niliwajibu kuwa ‘hapana’ kwa hivyo walikwenda kwa shemeji yangu na kumwambia, ‘amekataa kuongea na sisi.’

“Kuongeza kwenye suala la kulazimishwa, wanawake wa Yazidi waliishi katika kambi ambazo walizitegemea, na kwa hivyo walihisi kuwa na wajibu wa kufurahisha watoa huduma za kibinadamu, wafanyikazi wa kambi, na wanahabari ambao wote walitoa shinikizo kwa wahasiriwa kuhadithia visa vyao.”

Kwa sababu ya wanahabari kuangazia kisa hicho, kulikuwa na uwezekano wa kuongezeka kwa unyanyapaa wakati habari zilitolewa kwa msisimko kwa kutumia vichwa vya habari kama vile, “Mwanamke wa Yazidi aliyeshikiliwa kama mtumwa wa ngono kwa   miezi mitatu na ISIS na kubakwa na genge azungumza kuhusu mateso ya kutisha”; “ISIS inauza wasichana watumwa wa ngono kwa ‘bei kidogo kama pakiti ya sigara'” na “Wanawake wa Yazidi wanafanyiwa shunguli za matibabu ili “kurudisha ubikira” baada ya kubakwa na Daesh.”[b]

Rasilimali Za Ziada: Usalama

Kuna miongozo anuwai ya kuweka salama kwenye kazi hatari zilizochapishwa na mashirika ya msaada wa vyombo vya habari na mashirika ya ulinzi. Tungependekeza kuanza na muhtasari uliotolewa na CPJ (Kamati ya Kulinda Waandishi wa Habari), Muungano wa ACOS (Utamaduni wa Usalama) na Rory Peck Trust (iliyoundwa kwa wafanyikazi huru), lakini kuna rasilimali zingine nyingi zinazofaa. (Mashirika yale yale pia yanaweza kushauri juu ya kupata mafunzo na aina zingine za msaada).

Salama na salama kutoka Jumuiya ya Doc imeundwa kwa watengenezaji wa filamu. Mbali na kutoa vidokezo juu ya usalama wa mwili, inatoa ushauri muhimu sana ambao utakuwa muhimu kwa mwandishi wa habari yeyote juu ya kuwalinda washiriki wa timu na wachangiaji kutoka vitisho vya usalama vya dijiti na dijiti - mambo mawili muhimu ambayo mara nyingi hupuuzwa. Mtandao wa Uandishi wa Habari za Uchunguzi wa Ulimwenguni pia unatoa ukurasa huu wa kina wa rasilimali.

Na ikiwa wewe ni mhariri au meneja, hakikisha uangalie zana ya tathmini ya usalama ya ACOS kwa mashirika mapya na mwongozo wa Kituo cha Dart cha kufanya kazi na wafanyikazi huru walio wazi kwa kiwewe. Frank Smyth kutoka CPJ ameandika ambayo inazungumzia hatari kwa waandishi wa habari wakati wa kufunika CRSV.

Maelezo ya chini:

  • a

    Tazama: https://www.cjr.org/analysis/rohingya-interviews.php

  • b

    Johanna E. Foster na Sherizaan Minwalla, 'Sauti za Wanawake wa Yazidi: Maoni ya Mazoea ya Uandishi wa Habari katika Kuripoti juu ya dhuruma, Ukatili wa Kijinsia wa Isis,' Mkutano wa Kimataifa wa Mafunzo ya Wanawake 67 (2018): 53-64.